Sunday, February 7, 2016

KIDAGAA SURA YA TISA

SURA YA TISA
Alidhania hawezi kufa hata alipowadhalimu na kuwatesa wananchi wasio na hatia. Akaanza kupanga mazishi yake huku ajihisi marehemu. Siku moja kamwita Amani na kumpa sururu, jembe na sepetu. “nataka uchimbe hapa kaburi langu. Siku nitakapokufa nataka kuzikwa hapa.” (uk 128) Ingawa Amani hakulitegemea, akawa hana budi ila kukamilisha jukumu lake. Hivyo basi, akalichimba kaburi hilo kwa siku tatu, likawa la fahari.
Mashaka kwake kukawa mashaka kweli, habebeki mwana wa watu. “Abwajabwaja ovyoovyo kama Mzee matuko Weye. (uk 129) Masomo keshaikatiza, nguo katupa na kuzura tupu mitaani. “Kumbe chema hakidumu.” (uk 129) Madhubuti amejitolea kutumikia nchi yake kwa moyo wake wote, tendo lililokuwa mkabala na alivyoamini baba mtu. “…alielewa fika kwamba ingebidi aukate mkono uliokuwa ukimlisha tangu hapo hata matokeo yake yakiwa nini.” (uk 130)
Mashaka akaleta rabsha na kuwazidi wafanyikazi wengine. Bi Zuhura akamwita Amani na pamoja wakamfungia Mashaka chumbani mwake. Kwa kuogofya yaliyokuwa yakiendelea, Bi Zuhura akamsihi Amani kalale ukumbini. Nyakti za usiku, Amani akaitwa na Bi Zuhura ili kaangalie ni nini kilichokuwa chini ya kitanda chake mama mtu. Ni katika harakati hizi ndipo Bwana Mtemi akarejea na kuwakuta wawili chumbani, wanatetemeka. “Ndani kukawa hakukaliki, nje hakutokeki.” (uk 131) “Kumbe huyu mwanamke huniendea kinyume na mfanyikazi jamani?” (uk 131) Akafungua sefu Mtemi, akatoa bunduki na kumshambulia. Alipodiriki kwamba Amani kaaga dunia, akambeba kwenye buti ya gari lake na kumtupa kando yam to Kiberenge, ambako aliokotwa na Wasamaria wema na kupelekwa zahanati ya Nasaba Bora.

Kukawa siku nyingi zimepita Amani akiwa zahanatini. Alipofumbua macho na kisha kuachwa huru, Imani wakaambatana na Majisifu kumpeleka kwake Majisifu mwenyewe. Amani kufika nyumbani, akakubaliwa kukaa katika “servants quarters” huku bado hawezi kuongea na kuwasiliana kwa kuandika. Imani akamchunga kakake vizuri sana.
Amani akamfahamisha Imani ya kuwa angependa kujistarehesha kwa kusoma vitabu. Imani akamwazimia vitabu kutoka kwa Mwalimu Majisifu, ikiwemo kimoja kwa anwani la “Kidagaa kimemwozea”. Kwa mshangao, kitabu chenye picha ndicho kile chake, mswada aliyorudishiwa kwa kuwa hauwezi chapika. Majisifu kajikuta taabani. “Lililomshangaza ni kwamba Yule aliyeitwa mwandishi na kupachikwa picha yake katika jalada la nyuma, hakuwa ndiye mwandishi wa kitabu hicho.” (uk 140) “…kilichokuwa chake kimekuwa cha mwingine.” (uk 141)
Amani akamwandikia Imani barua kumwelezea juu ya le aliyoyaona. Majisifu akaipata barua ile na kuisoma. Hapo Imani akampata na kumkabili vipasavyo. Majisifu akatoa zote siri alizokuwa amezibana, “Kumbe umdhaniye ndiye siye?” Akamwandikia karatasi ndogo Amani kwa Majisifu.
Share:

1 comment:

  1. Betway Casino review for 2019 - Dr.MD
    We have the latest 충청북도 출장마사지 in 삼척 출장안마 the 남양주 출장샵 casino industry with all the latest in casino games, sports betting, casino 경상북도 출장마사지 promotions, free spins and more. Rating: 4.3 충청남도 출장안마 · ‎12 reviews

    ReplyDelete

Popular Posts

Unordered List

Pages

Categories

Labels

Download

Powered by Blogger.

Footer Widget 1

Text Widget

Blogger Tricks

Blogger Themes

Categories

Copyright © MWONGOZO NA UCHAMBUZI WA FASIHI ANDISH | Powered by Jkts Company 0706509638 |