SURA YA NNE
“Siku tatu tangu Imani kende kwa nduguye nab ado
hajaonekana.” (uk 49) Dora hakuweza kuvumilia kuwa linda wanawe.
Akazidiwa hamaki na kumshambulia mumewe Bwana Majisifu ambaye kajibu kwa
“kumfungulia cherehani ya matusi” (uk 52).
Hata hivyo, majibizano
hayo yanakatizwa ghafla mlango unapobishwa na mpwa wake majisifu,
Mashaka bintiye Mtemi Nasaba Bora. Majisifu na Dora wanavua nyuso za
hasira na kujibandika za bashasha, anagalau mgeni asijejua siri za
jirani. Haisuru, wanaingia katka gumzo, ambapo Mwalimu Majisfu hachoki
kumkosoa Mashaka.
Baada ya Dora na Mashaka kujiburudisha kwa chai,
iliyosusiwa na Majisifu, kwani siku hizi kakosa tumbo la kuikarisha,
sababu yenyewe keshazoea sharabu. Ndipo Mwalimu Majisifu anamwuliza
mpwake kazi ambayo angependa kufanya baadaya ya masomo. “Napenda niwe
mwandishi wa vitabu kama wewe amu”, (uk 47) akajibu Mashaka. Kwa
kumalizia, Majisifu akaboronga lugha, “Kitanda usichokilalia hukijui
kunguni wake” (uk 47).
Acha mashaka aulizie muda aliouchukua mwalimu
Majisifu kukiandika kitabu chake cha “Kidagaa Kimemwozea”, jawabu likawa
kaski mosi. “Aha, kurasa zote hizo?” akaendeleza mashaka. “Mwandishi
bora lazima aandike haraka kabla mwazo hayajayeyuka kuwa upepo (uk 48).
Anapoondoka Mashaka, anampasa Mwalimu Majisifu barua inayomwalika
Wangwani ili kutoa mihadhara kuhusu uandishi wake. Anamfahamisha Dora
ambaye baada ya kuomba kuletewa “rinda na viatu toka Mkokotoni”, anaanza
tena kushambuliana. “Kama utaweza, mbwa apige mswaki.” (uk 51).
Anaghadhabika Mwalimu na kijibu kwa matusi. Hata hivyo tunajulishwa
kwamba “nyoko nyoko” zilikuwa shibe za kawaida kwao.
Amani na Imani
wanastakimu pamoja wakiwa na mwano wa kupagazwa, Uhuru. Hapa ndipo
tunaelezwa vile wawili hawa walivyokutana na pia yale yaliyowatokea.
Nyakti ni za usiku usiku, kuamkia sikukuu ya Uhuru. Wanasokomoko
wengine, lao wanalo kushehekea kwa nyimbo na ngoma.
Mwinyihatibu
mtembezi ambaye alikuwa mfanyikazi wa Mtemi alinunua shamba kule Baraka,
alikoishi na familia yake akina Imani. Basi baba alipofariki, wakaja
Askari na kudai kuwa sehemu ile ya ardhi lilikuwa na mwenyewe. Kupinga
walipigwa na kuachwa hali mahututi. Oscar Kambona akatorokea na kudai
kuja kulipiza kisasi. Baada ya mama mtu kuzikwa, wakaja Askari na
kuchoma maskani ile, nusura Imani ateketee.
Marejesho hadi mwanzo wa safari hii ya waja hawa waili. Wanapokutana
kando ya ziwa Mawewa, tunapomwona kijana mmoja, umri wa miaka isghirini
hivi anaposoma hatujui nini. Kisha anaitupa runda ile ya makaratasi
baharini. Kumbe ilikuwa mswada ambao Amani kapeleka ili
kuchapishwa,akarudishiwa kwa madai kwamba haikuwezekana kuchapishwa.
Kumbe Amani kachezewa karata, mswada wake ukaibiwa na kuchapishwa kwa
jina la Majisifu Majimarefu. Hapa basi tunashangazwa kuona kwamba ni
wale wanaofaa kuwa kiegezo kwa wnagenzi, ndio wanaobadilika kuwa paka
kulinda kitoweo.
Wakati ambapo walikuwa wakipiga gumzo usiku kucha,
mtoto Uhuru alilala fofofo. Ndugu hawa wa kupanga, wasiojuana, wazaziye
Uhuru, mtoto wa kupagazwawakavuliana siri zao. Hata Amani aliyekuwa
msiri kama kaburi hakuwa na jingine ila kudondoa alicho nacho rohoni.
0 comments:
Post a Comment