Sunday, February 7, 2016

MWONGOZO WA KIDAGAA SURA YA PILI

 SURA YA PILI

Eneo la Sokomoko ambako ni kwa matajiri. Kitambo kabla ya Uhuru, eneo hili lilikuwa limetengewa Wazungu pekee. Wamiliki walipanda mimea tofauti tofauti ikiwemo pareto, alizeti na kadhalika. Weusi hawakuruhusiwa kuishi wala kulima mazao yoyote yaletayo fedha. Mweusi angefuga tu mifugo ya kienyeji lakini njee ya Sokomoko.
Matajiri wa Sokomoko waliyanyaka ardhi zile zilimilikiwa na wakoloni ambao walirudi makwao. Miongoni mwa Wazungu hao, Major noon almaarufu Majujnuni ambaye shamba lake lilinyakuliwa na Nasaba Bora, kaacha nyuma kasri moja kubwa alililokuwa amejengea mpenziwe Michele ili wakaishi pamoja.

 Mara yake ya kwanza kuja Afrika baada ya vita vya pili vya dunia, Majununi kajenga hema na kasha kumwalika mpenziwe Michele. Kidosho huyo kafika, akakataa katakata kushuka toka kwenye ndege na kumwambia Majununi kwamba hawezi katu kuishi mwituni kama mnyama. Akaabiri ndege na kurudi kwao Ufaransa. Kujenga nyumba yenye viumba vinne, Michele kanengua kuwaq kamwe hawezi kuishi ndani ya kibanda. Majununi akawa mtaftaji asiyechoka, ila akichoka, basi huwa keshapata. Kajenga basi kasri kubwa lenye viumba kumi na vitatu. Asiyetosheka na la ninaye, kumbe la mweziwe maradhi. Mara hii, kidosho kashuka na kuingia mle kwenye kasri, vyumba kumi na vitatu? Bahati mbaya. Sakafu yenye rangi nyekundu? Hatari, na mbona madirisha makubwa.

“Monsieur Noon, naomba radhi sana lakini hatufaani. Pengine imeandikwa kwamba tusioane. Narudi kwetu. Katafute mwanamke kufu yako.” Ndiyo maneno yake Michele kabla ya kuabiri ndege na kurudi kwao.
Akakosa hata tone moja la mahaba rohoni kwa wanawake wote Majununi, na kasha kaingilia ukulima na ufugaji kwa moyo, acha roho. Hata hivyo kwenye bamba la zege karibu na dohani ukumbizoni kaandika, “Your beauty is my weakness”, maneno yaliyobaki kuwa ukumbusho kwake kuhusu mapenzi yake kwa Michele.

Mteni Nasaba akiwa kwenye Wizara ya Ardhi kajitengenezea stakabadhi alizozitumia kunyakua shamba la mwajiri wake. Akawa Mtemi, mkubwa, nusu mungu sijui nini. Watu wakawa ni kufyata ndimi dhidi ya dhulma zake Mtemi. Akawa wa kuvunja wale waliodhubutu kumpinga na kuckichukua akitakacho. Kwake hoja ikawa kupata alichokitafuta, wala si jinsi ya kukipata.
Kwake Mtemi usafi zaidi kukawa balaa. Vitu vikuukuu, hela hatumii hajali. Machweo wakafika akina Amani kwa Mtemi. Wakampata kamsimamia fundu aliyekuwa akibambanyabambanya katika injini. Kawatupia jicho la dharau na kuwauliza maswali za upumbavu. Akawakodolea macho na kushangazwa na jawabuye Imani, aliyemtizama kwa kumkazia macho Mtemi havumilii. “Usinivue nguo kwa macho yako wee!” (uk 21).
Akawaaga baada ya kumsukuma kidogo, eti aenda “kusukuhisha mgogoro wa shamba…” (uk 21). Akatokomea hukoo!
Basi DJ kamfikisha Amani kwa Bi Zuhura, mkewe Mtemi Nasaba Bora. Amani akawa akisubiri kuonyeshwa makazi yake, kwenye kibanda la wafanyikazi, la makabwela kama yeye. Kufuka nje kwa Imani na DJ, jibwa lile jeupe, aliyedhoofika na kung’ookang’ooka ngozi haliachi “kubweka bwe bwe, bweka ubweke kufa kwaja.” (uk 24) akamwonea huruma DJ na kuuliza kwa nini kwa nini lisiachwe “free maze”.
Akakumbushwa na Bi Zuhura asiwe “kama wazungu wanaopaswa kukumbushwa kwamba mbwa ni ni mnyama”. Kukawa tayari kumeingia machweo walipotoka akina DJ.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Popular Posts

Unordered List

Pages

Categories

Labels

Download

Powered by Blogger.

Footer Widget 1

Text Widget

Blogger Tricks

Blogger Themes

Categories

Copyright © MWONGOZO NA UCHAMBUZI WA FASIHI ANDISH | Powered by Jkts Company 0706509638 |