Sunday, February 7, 2016

KIDAGAA SURA YA NANE

SURA YA NANE
Ikuluni kwa Matuko Weye kaja askari mmoja na redio aliyoitazamia kusikiliza matangazo ya mpira baina ya timu za Songoa FC na Meza Wembe kutoka Wangwani. Wakawa wote, askari na waziri, Amani na Imani wanayasikiliza matangazo hayo kwa njia mwafaka kabisa.
Mpira karibu kumalizika, Songoa ikabahatika bao moja kutoka kwa mchezaji mmoja maarufu kwa jina la Chwechwe Makweche almaarufu “Horsepower”. Imani akajikuta katikati ya fahamu, hajui amshangilie kakake kwa kuifunia Tomoko ama ahuzunike kwa kakake kuwasahau kabisa.
Kidogo kukasikika mngurumo wa gari. Mtemi Nasaba kafika na kuwaamuru askari, “Wafungulieni hawa washenzi watoke.” (uk 109). Wakawa huru Amani na Imani. Lakini tujiulize, kwa nini wakaachwa huru bila kushtakiwa? Ndio wanyonge hupitia, wasio na lao, hawana mbele wala nyuma.
Kuondoka kwake Majisifu kuelekea Wangwani kulisadifiana na kurudi kwake Madhubuti kutoka Urusi. Huku Amani na Imani wamesharudi kazini, Amani akatunga beti kuhusu mwanawe wa kupanga, Uhuru. Baadaye akajaribu kutunga nyingine kwa heshima ya rafikiye DJ, akashindwa, kwani maneno hayakuitwa yakaitika. Twaona kwamba DJ kafikishwa zahanati ya Nasaba Bora baada ya hali yake kuwa mbaya, huku adinda kunengua kilichokuwa kimemsadiki.
Miaka mingi baadaye Imani kamsihi Amani iiandike tawasifu kuhusu maisha yake, hakukosa kudukia yaliyomo baina yake na Madhubuti. Walikuwa masahibu wa chanda na pete, hata wengi walishangazwa alipohamia Madhubuti kibandani mwake Amani.
Wakawa wamepatana. Madhubuti akiwa tayari kwa mapinduzi naye Amani akiwa tayari kupiga jeki. Mtemi haelewi yaliyomkuta mwanawe. Madhubuti alipoajiriwa Songoa, wakawa wanawasiliana kupitia nyaraka. Madhubuti akawa marafiki na maofisa wa wizara ya ardhi kwa lengo la kupasua mbarika alikotokea Mtemi kumiliki mashamba mengi na makubwa makubwa kama vile.

Tangu Mashaka kupata barua toka kwa Ben Bella, akawa “mnuni,kama kondoo” (uk 121). Aliathiriwa sana na yale yawapatayo waliowachana kimapenzi. Akakatiza masomo na kurudi nyumbani. Juhudi za wazaziye kumsihi akarudi skulini zikaambulia patupu, mtoto akawa kisiki hasikii.
Majisifu naye akafika chuo kikuu cha Mkokotoni kulikojaa sisisi, macho kama elfu za na zaidi. Akakaribishwa na kasha kupewa nafasi akahutubu. “…alikumbwa na kiherehere na kohoro.” (uk ) Ahaa! Mambo yanamwendea zegemnege. Akafungua mkoba wake huku kijasho chembamba kinamtoka. Akaangusha karatasi zake kutokana na uoga na kiwewe. Akarudi na kuketi chini huku umati ukiangua kicheko.
Baada ya mhadhiri mmoja kunong’onezana naye kwa muda, ikasemekana kwamba hangeweza kuhutubu moja kwa moja, basi ikabidi wahadhiri waulize maswali huku Majisifu akiyajibu. Akaulizwa kwa nini akachagua anwani “Kidagaa Kimemwozea” kwenye kitabu chake. “Kwa kweli sijui ee, sijui kwa nini nilchagua kukiita kitabu hicho, Kidagaa Kimemwozea. Niligutuka tu nimekiita hivyo.” (uk 123)

La pili akaulizwa maoni yake kuhusu jinsi mataifa ya Afrika baaada ya mkoloni. “Kuna umoja na utangamano humu barani. Viongozi wa Afrika huru wameshika usukani kwa njia bora zaidi. Afrika imekombolewa toka kwa matatizo ya njaa, umaskini na ujinga.” (uk 123-124)
Akajikuta hawezi kujibu maswali kwani majibu yake yalitfautiana sana na maoni yake kwenye “Kidagaa Kimemwozea”. Akajitetea, “La! Mimi sikuonyesha hivyo kamwe katika riwaya hiyo.” (uk ). Basi nani kaonyesha, na hata hivyo, yanaonekana hata Mwalimu Majisifu hakuwa amekisoma kitabu hicho.
Wahadhiri wakashangazwa hadi ya kushangazwa. Swali akalipata kuhusu hali ya Kiswahili. Akajibu, “Kiswahili kitaendelea kuimarika vyema lakini sharti tuondoe Watanzania na Wakenya kwenye ulingo…Watanzania wanadhania kwamba ni wao tu ndio wakijua Kiswahili na Wakenya wanafikiria kwamba kulipua makombora ya misamiati…” (uk 125) Kukalipuka kicheko.
Akaulizwa ikiwa kaandika riwaya ya “Kidagaa Kimemwozea” na kwamba kulikuwa na fununu kuwa kauchukua mswada wa mtu mwingine. “hayo yalikuwa mno.” (uk 125) Akafyata ulimi, huku unga umemzidi maji. Hata hivyo akaokolewa na mhadhiri mmoja aliyedai kuwa hotuba ingeendelea siku iliyofuatia.
Jioni hiyo, Majisifu akaabiri ndege kurudi Tomoko huku yu tayari kulipa fidia ikibidi. Akajikuta “atokwa na machozi kama mtoto mdogo.” (uk 127) Akajuta Majisifu, kumbe kidagaa kilikuwa kimemwozea.
 

Share:

0 comments:

Post a Comment

Popular Posts

Unordered List

Pages

Categories

Labels

Download

Powered by Blogger.

Footer Widget 1

Text Widget

Blogger Tricks

Blogger Themes

Categories

Copyright © MWONGOZO NA UCHAMBUZI WA FASIHI ANDISH | Powered by Jkts Company 0706509638 |