SURA YA SABA
Siku tatu baada ya Mtemi kupokea barua kutoka kwa
mwanawe Madhubuti, majira ya saa tatu asubuhi, kakake Mwalimu Majisifu
akamtembelea kwake katika kasri la Majununi. Kukawa siku hizi, mkewe Bi
Zuhura katafunwa na jakamoyo na upweke juu ya mumewe asiyesemezeka wala
kuambilika. Kukawa Mtemi hawezichelewa kusuluhisha migogoro ya mashamba
yake yasiyoisha.
Majisifu akapokelewa na Bi Zuhura wakawa wanapiga
gumzo sebuleni. Alipotoka kukoga Mtemi, akavalia kwa muda, hajali
kumsabahi. Baadaye akajitosa ukumbini aliposikia kakake kaulizia aliko.
Bi Zuhura akawapa nafasi baada ya Mtemi kukaa mbali sana na wote wawili,
Majisifu na Zuhura. Kimya kirefu kikajiri baina yao.
Alipojirudisha
Mtemi, akamwuliza kakake majisifu kwa nini kakosekana mkutanoni.
Majisifu naye akajibu kwamba kawa ameenda “ibada”. Akamwonya kakake
Mtemi kuhusiana na madhara ya pombe, sana ikilinganishwa na vile baba
yao kasisi kawakuza. Kujitetea majisifu akadai kwamba uovu uliofichwa
ndani ya dini haumpendezi. “Afadhali nitende mambo yangu waziwazi.´(uk
93)
Mtemi akawa anampozoa Mwalimu hasira huku anajizuia kupasuka. Alipodai
kujali maslahi yake Majisifu, akamwambia ajali maslahi ya Wanasokomoko
wote. “Kama ungekuwa unajali maslahi yaw engine, yule mchungaji wako na
mtumishi wangu hawangekuwa wanapigwa na baridi kule ndani kwa kosa
ambalo hawakulitenda.” (uk )
Chai ilipoletwa mezani, Mtemi akashangaa
kuona ni ya mkandaa. Akawa hana jingine ila kuinywa ili kuficha ukweli.
Ndipo akagundua ndani mna nzi mkubwa wa buluu, kakufia mle ndani.
Twaona kwamba haya yote ya suintofahamu katokana na kitiwa kwa Amani
mbaroni. Wakawa hawaongezani wala kusemezana. Kukawa kimya.
Yalipozidi
unga, Majisifu akaaga na kutokomea mbali, ukuta wa uhasama ukakithiri
baina yao. Lakini kitu kimoja walichokosa kujua ni kwamba siku hiyo kawa
mwisho wa kukutana kwao katika kasri la Majununi. Hatujui kukatokea
nini baadaye ila tu tusome. Kutoka kwake Mtemi bila kwaheri, Majisifu
akahesabu boriti kuelekea kwa Mama N’tilie alikotarajia kuwa na ibada.
Akakumbuka
kwamba alikuwa na kipindi kimoja cha kufundisha lakini akadai kuwapa
nafasi wale maziwa lala wakawaandikie muhibu wao barua za mapenzi na
kupanga jinsi ya kukiuka vizingiti vya shule.
Hapa twajagundua kwamba
Mwalimu Majisifu hakuwa na akili nzuri ya kumwezesha kuandika vitabu.
“Ningekuwa na akili nzuri ya kuandika kitabu ningeandika juu ya kibe
wachezacho wasichana hao na mwalimu mkuu…” (uk 98)
Akaitisha bibilia Mtemi na kuanza kusoma, kitu alichokawia kufanya miaka
nenda miaka rudi. Akakumbuka kuhusu kidoshao kimoja kiguru aliabiri
naye gari pamoja kuelekea mjini. Akajitetea Nasaba lakini kakosolewa
kwamba hangeweza kucheza ngoma ile hata kama ni yeye aliyeianzisha.
Kutia nanga mjini, Nasaba akamwona Yule mrembo akiinama na kutoa
mikongojo miwili ya kwapani. Akagundua ukweli, upendo ukamtoka, akaomba
radhi na kutokomea.
Na katika harakati hizi ndipo kukasikika ukwenzi
mkali kutoka nje. Alipotazama Zuhura ili kutendua kilichosadiki,
akamwona DJ yu chini huku mguu wake uking’atwa na mbwa Jimmy. Zuhura
akamcharaza Yule mbwa na akatoroka asionekane tena. Akampokeza barua ile
Bi Zuhura na kuomba kuondoka ili kupeleka ng’ombe wa mwajiri wake
malishoni.
Basi mkewe Mtemi akamfikishia barua yake, hapo ndipo
pakatokea mzozano baina yao Zuhura alipomwonya Mtemi kwa kutowachanja
mbwa wake wakti akiwahukumu wale waliokosa kuwachanja wao. Kwa madharau
akadai kwamba DJ alistahili alichokipata.
Kufungua barua ile,
akakutana na yalimshangaza. Lowela akaonya kutoboa siri Mtemi akosapo
kuwaachilia huru Amani na Imani. Ndiyo mapenzi ya masharti yake binti wa
watu. “Moyo ulimpapa na kijasho chembamba juu ya mwanzi wa pua. Akahisi
uchungu wa mwiba wa kujidunga.” (uk 106) Atahadhari huku maji
yashammwagikia? Nani atakayeyazoa?
0 comments:
Post a Comment