Sunday, February 7, 2016

KIDAGAA SURA YA TANO

SURA YA TANO
Uwanja wa Nasaba Bora ambapo wananchi wansherehekea sikukuu ya Wazalendo umefumukana hadi ya kufumuka. Wameroa kwa jasho kutokana na joto jingi. Waliomo, wananchi wa kawaida hawakuchelewa kufika, saa tatu upuzi walikuwa wamefika. Acha viongozi waje wakti wao na kufika pao, walipotengewa.
Mwendo wa saa tano unusu, anafika Mtemi na aina yake. Jukwani anapanda Balozi, jamaa mcheshi na mjanja. Anayo matamu matamu yanayoweza kumtoa nyoka pangoni. Hata hivyo, anajihadhari asije akaukate “mkono uliokuwa ukimlisha au kuziuma chuchu alizozinyonya”. (uk 67)
Ingawa Balozi ni mtu aliye na ushawishi mkubwa kwa umati, hakosi kuonyesha uzembe wake kwa kumsifu Mtemi, sifa zilizo kinyume kabisa na matendo yake Mtemi Nasaba Bora. Anapowauliza wananchi ikiwa kunaye yeyote asiyempenda Mtemi, kimya kinawazidi wasiweze hata kohoa. “Anatambulikana kwa fadhili na utu wema wake…Kiongozi aliyeteuliwa na Mwenyezi Mungu.” (uk 68) Angurumapo samba, mcheza nani? Hakuna aliyethubutu ila wengine kama Mzee Matuko Weye. Hata hivyo hatukosi wale wa kunung’unika kichichini angalau wasije wakapatikana na Askari wake Mtemi, Bi Kizee akiwemo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Popular Posts

Unordered List

Pages

Categories

Labels

Download

Powered by Blogger.

Footer Widget 1

Text Widget

Blogger Tricks

Blogger Themes

Categories

Copyright © MWONGOZO NA UCHAMBUZI WA FASIHI ANDISH | Powered by Jkts Company 0706509638 |